Header Ads

Beki wa FC BARCELONA arejea kikosini kuivaa Athletic Bilbao

Barcelona, Spain

Na Kalunde:
Beki mahiri wa miamba wa Uhispania, FC Barcelona, Jordi Alba anatarajiwa kuingia kikosini baada ya kuwa nje ya uwanja kwa majeraha ya paja aliyoyapata kwenye mazoezi mapema mwezi huu.

Mhispania huyo akiwa anaugulia maumivu hayo, amekosa mechi tatu ambazo ni FC BARCELONA dhidi ya Olympiacos, Malaga na Murcia (ilikuwa mechi ya Copa Del Rey). Amerudi kwenye mazoezi Jumatano wiki hii na anatarajiwa kuivaa Athletic Bilbao hapo Jumamosi.

Jordi Alba returns

Msimu huu, Jordi Alba amecheza jumla ya mechi 11 kabla ya kupata majeraha hayo na nafasi yake ilikuwa inachukuliwa na Lucas Digne.

Kwa ujio wake Alba, Meneja wa timu hiyo Ernesto Valverde atakuwa na chaguzi sasa juu ya beki hawa. Lakini pia inasemekana Jordi Alba anafurahia sana kwenye uongozi wa kocha huyu mpya baada ya Luis Enrique.

Tembelea www.kalunde.co kwa habari mbalimbali pia

No comments: