ZITAMBUE AINA ZA WAKE KATIKA FAMILIA, KISHA TUAMBIE AINA YA MKE WAKO.
10 TYPES OF WIVES
1. Mke sherehe (Party wife.)
Wake wa aina hii wako mguu na njia kila siku na wanajuana na kila mtu. Wao kila siku wana sherehe, leo sendoff, kesho kichen party, keshokutwa bag party mtondogoo wedding nk. Mara chache wanakaa nyumbani siku za wikiendi, yani zile siku za mume na watoto kuwepo nyumbani yeye ndio party mood activated. Wanaweza kutumia hela ya chakula cha familia kuchangia sherehe au kununulia zawadi.2. Mke kamusi (Dictionary wife
Hahitaji kuomba ushauri hata siku moja yeye anachojua ndio mpango mzima. Kila wakati analazimisha mawazo yake yawe sawia na yaaminike. Hataki kupingwa au kurekebishwa kwa chochote. Anatoa oda tu, neno naomba au tafadhali hutolisikia kwake, na ni mkali sana vitu vinavyopotea au kuwekwa vibaya nyumbani tofauti na alivyovipanga yeye.3. Mke pampas (Pampas wife)
Huyu ni mke aliyeharibiwa kabisa na wazazi wake hususani wazazi matajiri, wazazi wanaojiweza, au labda ndio binti pekee kwao. Wavivu sana kufanya kazi za nyumbani. Wao wanapenda tu shopping na vitu vya fasheni. Maranyingi mke huyu anamwona mume wake kama house boy, utaskia baby nisaidie hiki, baby niletee kile, hubby njoo nitolee hiki, hubby utanipeleka pale. Mume utadhani dereva au shamba boy. Unakuta mume anahasira moyoni lakini ndio hivyo tena kamba ilishaungulia kiwandani.4 Mke ofisi (The Office wife)
Mke wa aina hii anajali sana majukumu ya kazini kuliko familia yake, anaweza kuwa na muda mrefu sana wa kazi akakosa muda na watoto au mume wake na anatumia majukumu ya kazi kama kisingizio cha kutokuwepo nyumbani au kutotimiza majukumu yake ya mke au mama nyumbani. Ningumu sana kwa mke wahivi kumheshimu mume wake, na hawa ndio wanaowafanya wanawake wengine waliosoma kuonekana wabaya kwenye ndoa. Mawazo yao nikwamba mume hana umuhimu sana maana hata wao wanaweza kuendesha familia bila shida. Waume wanaoishi na wake wa aina hii wanastahili pole na uvumilivu mkubwa.
5. Mke mgonjwa (sick wife)
Wakati wote anaonekana kama anaumwa, mpole sana na aliyenyong’onyea. Anapenda kulaumu kila kitu, atalaumu kuhusu mume, watoto, ndugu hata hali ya hewa. Kila wakati wao ni wenye hofu kwa kila kitu, ukimshauri afanye bishara hii anaogopa mwambie nyingine ataogopa, anaweza kulalamika uchovu au kuumwa hata katika nyakati mume anaomba tendo la ndoa. Pamoja na lawama za udhaifu na kuumwa au kuchoka mara kwa mara wala hauoni akisema anaenda hospitali.6. Mke mwalimu mkuu (Headmistress wife)
Hawa hujiweka kuwa viranja wa familia hatakama mume ndio anayeleta kila kitu. Kila wakati anatamani aonekane yeye ndio kiongozi wa familia. Maranyingi huwafanya wengine wote ni watoto au wanafunzi bila kujali huyu ni mume wake au yule ni mgeni kaja kutembelea familia. Wanauliza maswali kwenye kila kitu, utaskia, kwanini umefanya hivi, kwanini hiki kiko pale, kwanini hivi kwanini vile na pia wanaweza kutoa adhabu hata kwa waume zao kwa vitu visivyo vya maana kabisa. Utaskia “umeamua kufanya hivyo ee!! Basi utaona.7. Mke ngumi (fighting wife)
Wake wa namna hii ni wenye kuudhi kila mara na pia mara kwa mara ni wapenda fujo. Anawezakuweka mazingira ya valangati hatakama haukuwa na mpango wa kurusha ngumi ukajikuta mmekunjana, akianza fujo hajali umelala, umepumzika, unaongea na simu, unakula, uko na marafiki, hilo hajali we fahamu tu inakula kwako hadi hasira zake ziishe. Wanapenda kupayuka sana, atarusha maneno kwa sauti ya juu tena maneno yaliyounganika kama vile taarabu na kama ndio mnaishi uswahilini kila jirani atajua kimenuka kwenu. Akianza kuongea hanyamazi, bora nyuki au mbu masikioni kuliko mke wa aina hii. Wake wahivi wanaamini sana kwenye nadharia ya moto kwa moto, ukimwaga ugali anamwaga mboga.
No comments:
Post a Comment